Kitabu hiki kinafanya tathmini ya kina ya urais wa Dokta John Pombe Magufuli, Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tangu alipoingia madarakani Novemba 5, 2015 hadi Novemba 5, 2017. Kitabu kinaangalia maeneo ambayo Rais Magufuli amefanya vizuri na yale aliyofanya vibaya. Ni uchambuzi makini usioelemea upande wowote isipokuwa kwenye ukweli.